Wednesday, 27 January 2016

RAILA ODINGA

Kinara wa mrengo wa Cord Raila Odinga akishirikiana na baadhi ya viongozi wa mrengo wake wa kanda ya Pwani wameitaja barabara moja katika kaunti ya Mombasa jina la mwendazake mwanawe Fidel Odinga.


Ziara ya Raila mkoani Pwani inajiri siku chache baada ya kuhitimika kwa ziara ya Rais Uhuru Kenyatta katika kanda hiyo.



Thursday, 14 January 2016

ODINGA ON EURO SAGA

RAILA ODINGA NAMES ALLEGED BEHIND EUROBOND SAGA.

1. PATRICK KAMAU THUGE- NATIONAL TREASURY
2. BERNARD NDUNG'U
3. MOHAMMED NYAAOGA - CBK
4. PROF. NJUGUNA NDUNG'U - CBK
5. JOHN BIRECH
6. MOSES MUTHUI - CBK
7. HENRY ROTICH - CS TREASURY
8. JOSEPH KINYUA - STATE HOUSE.



Friday, 25 December 2015

KENYATTA NA FAMILIA YAKE WASHEREHEKEA KRISMASI MOMBASA


Rais Uhuru Kanyatta na familia yake akiwemo mke, mama, na watoto wake pamoja na seneta wa Nairobi Mike Mbuvi "Sonko"wamesherehekea siku kuu ya krismasi katika kaunti ya Mombasa.


Rais Uhuru ambaye ziara yake imekuwa ya siri mjini humo, amehudhuria misa ya maombi katika kanisa la Cathedral lililoko katika barabara na Nkruma jijini humo.



SHAMBULIZI LAMU


Wapiganaji wa Al- Shabab wamemuuwa polisi mmoja, baada ya bomu walilotega kulipuka muda mchache baada ya kupita lori la polisi kupita katika eneo hilo lililoko katika barabara ya Bodhei iliyoko katika kaunti ya Lamu.

Inaarifiwa maafisa hao walikuwa wanaelekea katika eneo la Bodhei lililoko katikati mwa kaunti ya Lamu na Garissa kabla ya tukio hilo kutokea.

                                     

KRISMASI


Wakristo kote ulimwenguni wameungana na waumini wengine katika sherehe za kuzaliwa kwa Yesu Kristo kulingana na maandiko ya dini yao.

Viongozi wa dini hiyo wamehubiri kudumishwa kwa amani, kuzidisha upendo pamoja na kumcha Mwenyezi Mungu ili kuzuia  Mashambulizi yanayotekelezwa na magaidi.


                                 

Wednesday, 23 December 2015

IEBC

Tume ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC imetangaza tarehe ya uchaguzi mdogo wa Useneta wa kaunti ya Kericho na Ubunge wa Malindi kaunti ya Kilifi kufanyika Machi ya tarehe 7 mwaka 2016.

Wakati huo huo maspika wa mabunge yote mawili Justin Muturi wa bunge la kitaifa na mwenzake Ekwe Ethuro wa Seneti, wametangaza rasmi uwazi wa viti hivyo viliwi.




Viti hivyo vilisalia wazi baada ya aliyekuwa seneta wa kaunti hiyo Charles Keter na mbunge Dan Kazungu kuteuliwa kuwa waziri wa Kawi na Madini mtawalia.

Sunday, 20 December 2015

HOFU ZA BOMU


Abiria waliokuwa wameabiri ndege ya AIR FRANCE iliyosajiliwa kwa nambari 463 iliyokuwa ikielekea nchini Mauritius kutoka France, wamelazimika kushuka ghafla katika uwanja wa ndege wa Moi mjini Mombasa, baada ya kupatikana kilipuzi ndani ya choo cha ndege hiyo.

Abiria 473 waliokuwa ndani ya ndege hiyo wamesalimishwa na kufanyiwa ukaguzi alfajiri hiyo ya saa 2:00, huku wanajeshi wa maji Kenya Navy na maafisa wa kutegua mabomu wakifanikiwa kuwatia mbaroni washukiwa wawili.

Waziri wa Usalama Joseph Ngaissery na msemaji wa polisi Charles Owino wametoa kauli zao kufuatia kitendo hicho cha kigaidi.